RAIS wa Shirikisho la Soka la Saudi Arabia, Yasser Al-Misehal, ametangaza kujiuzulu wadhifa wake kufuatia kushindwa kwa timu ya taifa ya Saudi Arabia kufuzu hatua ya mtoano katika Kombe la Dunia la 2026. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Al-Misehal amesema matokeo hayo hayakuendana na matarajio ya taifa na mashabiki wa Saudi Arabia, akieleza kuwa anachukua jukumu la matokeo hayo kwa kuamua kuachia nafasi yake.
Saudi Arabia ilimaliza hatua ya makundi ikiwa na pointi mbili pekee baada ya kutoka sare katika michezo miwili na kupoteza mchezo mmoja, hali iliyoifanya ishindwe kusonga mbele kwenye hatua ya 32 bora ya mashindano hayo.
Kujiuzulu kwa Al-Misehal kunahitimisha uongozi wake wa takribani miaka saba katika Shirikisho la Soka la Saudi Arabia, huku shirikisho hilo likitarajiwa kuanza mchakato wa kumpata kiongozi mpya atakayeongoza mipango ya maendeleo ya soka nchini humo.