Zacharia Hans Poppe
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Idara ya Biashara jijini Dar es Salaam, imekataa ombi la kampuni ya ZH Poppe Limited na wasimamizi wa mali za marehemu mfanyabiashara Zacharia Hans Poppe la kutaka kuzuia Benki ya Biashara ya Tanzania (TCB) kuuza mali zilizowekwa rehani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Uamuzi huo uliotolewa na Jaji Arnold Kirekiano siku ya Jumatatu, 15 Juni 2026, unaipa nafasi benki hiyo kuendelea na hatua za kukokotoa deni linalozidi shilingi bilioni 7.4 kupitia mnada wa mali hizo, ikiwemo malori, matanki ya mafuta na Trela.
Katika kesi hiyo, waombaji walidai kulikuwa na udanganyifu katika uhamisho wa hisa na walitaka kuzuia utekelezaji wa mnada huo.
Hata hivyo, uamuzi wa Jaji Kirekiano umefikia kuwa madai hayo hayakuthibitishwa na ni masuala ya ndani ya kampuni, na kwamba waombaji walishindwa kutimiza masharti ya kupata azimio la muda (temporary injunction).
Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa na tovuti ya The Citizen, Hatua hii inafuatia benki ya TCB kudai kuwa mkopo uliotolewa kwa ZH Poppe Limited haukurejeshwa kama ilivyokubaliwa, jambo lililowalazimisha kuchukua hatua za kisheria za kurejesha fedha zao kupitia mali zilizowekwa dhamana.