Mchezo huu wa ufunguzi wa Kundi L utachezwa kwenye uwanja wa AT&T Stadium jijini Arlington, Dallas, Texas, uwanja wenye uwezo wa kuhudumia zaidi ya mashabiki 80,000 na paa linaloweza kufungwa na kufunguka.
Kundi hili pia linajumulisha Ghana na Panama, hivyo timu zote mbili haziwezi kumudu kuteleza kwenye mchezo wa kwanza. England wanakuja wakiwa wamefuzu kwa rekodi safi ya ushindi 8 kati ya 8 katika kufuzu Ulaya, wakifunga mabao 22 na kufungwa sifuri huku Croatia wakiwa pia hawajafungwa kwenye kundi lao la kufuzu. Kwa England, mechi hii inawakilisha nafasi ya kuanza safari ya kuondoa ukame wa miaka 60 tangu ushindi wao wa pekee wa taji hili mwaka 1966.
England wanaingia kwenye mchezo huu wakiwa na moja ya safu za ushambuliaji zenye kutisha zaidi duniani, wakiongozwa na nahodha Harry Kane aliyefunga mabao 61 kwa Bayern Munich msimu huu na anayewania Tuzo ya Ballon d’Or. Jude Bellingham anatarajiwa kucheza nafasi ya kiungo wa kushambulia nyuma ya Kane, wakati Bukayo Saka na Anthony Gordon wakitegemewa kutoa kasi kutoka pembeni.
Hata hivyo, safu ya ulinzi ina wasiwasi mkubwa John Stones anasumbuliwa na majeruhi ya mara kwa mara, huku Dan Burn akiwa na umri wa miaka 34, na hakuna beki wa kushoto wa asili katika kikosi. Kocha Thomas Tuchel anatarajiwa kutumia mfumo wa 4-2-3-1 au 3-4-2-1 unaobadilika, akisisitiza mashambulizi ya haraka ya vertikali.
Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi
Croatia wanakuja na kikosi chenye uzoefu wa ajabu, wakiongozwa na nahodha Luka Modrić ambaye ana umri wa miaka 40 na anashiriki Kombe lake la tano la Dunia baada ya kupona jeraha la kuvunjika kwa mfupa wa shavu alilopata Aprili. Mateo Kovačić na Ivan Perišić (36) wanaongezewa nguvu na vijana kama Joško Gvardiol (24) na Luka Sučić (23).
Croatia wanajulikana kwa uwezo wao wa kudhibiti tempo ya mchezo kwa kumiliki mpra kwa asilimia kubwa, na katika kufuzu Ulaya walikuwa na wastani wa umiliki mkubwa. Kocha Zlatko Dalić anatarajiwa kutumia mfumo wa 4-3-3 unaobadilika kuwa 3-4-3 wakati wa kushambulia, huku Modrić akiwa ndio “ubongo” wa timu yote.
England wanatarajiwa kuanza na Jordan Pickford golini; Reece James, John Stones, Marc Guéhi, na Nico O’Reilly ulinzi; Declan Rice na Elliot Anderson kiungo; Jude Bellingham kiungo wa kushambulia; na mbele Bukayo Saka, Harry Kane, na Anthony Gordon.
Croatia watategemea Dominik Livaković golini; Josip Stanišić, Joško Gvardiol, Duje Ćaleta-Car, na Borna Sosa ulinzi; Luka Modrić, Mateo Kovačić, na Luka Sučić kiungo; na mbele Ivan Perišić, Andrej Kramarić, na Bruno Petković. Kwa kuzingatia ubora wa mashambulizi ya England na historia England wameshinda mechi 3 kati ya 4 za mwisho dhidi ya Croatia, wakijumuisha ushindi wa 5-1 mwaka 2009.